inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 31 Machi 2018

MTAZAMO: HII ITAKUSAIDIA KUONGOZA

#HiiItakusaidiaKuongoza na Henry Kazula


Picha:
https://www.the1thing.com/
Ili kujenga Timu yenye ufanisi/mafanikio katika Shirika/Kampuni, nakubaliana kabisa na msemo wa wahenga usemao; "Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu", lakini ifahamike kuwa Nguvu ya Timu dhabiti ipo katika 'nguvu' na jitihada ya kila mmoja. Hatuwezi kusema kuna umoja wenye nguvu ikiwa wachache ndani ya Timu ni 'wadhoofu'. Hivyo, ili kujenga Timu yenye nguvu unapaswa kuangalia 'nguvu' (ujuzi/uwezo/utayari) binafsi wa kila mtendaji.

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza Blog



Alhamisi, 24 Agosti 2017

Workshop Redesign Your Business Harnessing Green Markets



Workshop Redesign Your Business Harnessing Green Markets: In a process to Resign Your Business in a Networked societyDigital Innovation...Remember Global market is shifting to Green with enormous opportunities.

You're Invited to attend this Workshop to be aware of;

1.Trending issues in a Networked society and Digital Innovation-Business perspective

2.Trending issues in Global Green Market-The future is Green with unprecedented opportunities.

3.Harnessing Green business opportunities to Green jobs creation and decent jobs

4.Networked society & Digital Innovation-Green business/Market nexus

5.Redesign your business model to Green Business Model(GBM)

Register Today:
+255 754 572 143
or Contact #TGBN Events Manager: Mr.Henry Kazula
e-mail: jielimishekwanza@gmail.com

Alhamisi, 1 Juni 2017

“AZIMIO LA KILIMANJARO” - “KILIMANJARO DECLARATION” LAIBUA HARAKATI ZA KUMKOMBOA MWAFRIKA DHIDI YA UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU, UVUNJIFU WA AMANI NA KUTOJALI UTU


Picha: Activista Tanzania
Kufuatia makubaliano ya Azimio la Kilimanjaro au Azimio la Arusha lilioboreshwa-“Kilimanjaro Declaration” la tarehe 23-24 Agosti 2016, washiriki 272  kutoka ndani ya nchi takribani 45 yakiwemo mashirika binafsi, asasi za kiraia,umoja wa wafanyabiashara, wawakilishi wa vikundi vya wanawake na wanaume, Vijana, watu wenye ulemavu, Wabunge na mashirika ya habari, na vikundi vya Dini na Waafrika waishio Nje ya Afrika walikuta Arusha,Tanzania kujalidili mustakabali wa Bara la Afrika linaloaminishwa kuwa ni masikini ilihali lina utajiri wa kutosha lakini watu watu wanaishi maisha duni yenye changamoto mbali mbali zinazohusiana na uvunjivu wa amani, kutojali haki na utu wao kwa maslahi ya wachache.
Mkutano huo mkubwa ulikuja na maazimio makuu sita (6) kama ifuatavyo;
1.    Afrika ina utajiri.Kuitambua Afrika na Kuwaaminisha Waafrika na Dunia kwa ujumla wake kuwa ni Tajiri na Utajiri huo ni wa watu wote na si kwa maslahi ya wachache kisiasa na kiuchumi.Hivyo kupambana kuleta maendeleo ya kiuchumi yenye kujali na kujumuisha maslahi ya kijamii na kujali Mazingira.
2.    Afrika ina vivutio vingi na vya kila aina, vyenye utajiri, hivyo hutosha kujiponya na kurekebisha uharibifu wa kikoloni dhidi ya Waafrika na Mazingira.Pia itambulike kuwa uafrika unamaanisha kuthamini utu wa wengine kupitia falsafa ya “Ubuntu” iliyo fahali na utu wa Mwafrika.
3.    Vijana wa Kiafrika ni msingi imara wa kujenga na kuleta mafanikio katika Bara la Afrika na ni chachu ya kuamsha na kuhamasisha wengine kujua haki na wajibu wa kutenda Haki, kuleta Amani na Kuheshimu wengine.
4.    Waafrika waishio nje ya Afrika bila kujali kuwa wamehamia huko ugenini; ikiwa ni kwa ajili ya utumwa, ukoloni au mfumo wa kisasa wa kuhama ili kutafuta maisha bora wana wajibu wa kutumia mbinu na ujuzi katika taaluma zao kuchangia harakati za kuwakomboa Waafrika wengine dhidi ya umasikini
5.    Waafrika tumejitoa kwa dhati kuwa wamoja, kwa ajili ya mustakabali wa Raia wema baadaye kuwa tutashirikiana kutoa msaada wa kuanzia ngazi ya chini, kuwajengea uwezo viongozi wa Serikali za mtaa na wanaharakati wa ngazi za chini ili kujenga hamasa na msukumo kwa jamii kutoka ngazi chini hadi kuvuka mipaka.
6.    Waafrika tumejitoa kujenga harakati za Kiraia zenye kubeba jukumu la la uwakilishi na kusimamia viwango vya ubora kiutendaji na maadili mema.
Kufuatia maazimio hayo (6) washiriki, kwa niaba ya Waafrika, waliona ni vyema kuanzisha Kampeni za kiuharakati kuanzia ngazi ya Serikali za mtaa, Kitaifa, Bara na Dunia kwa ujumla ili;
a.    kutanua wigo wa kuchukua hatua kuhusiana na masuala ya kijamii na Siasa,
b.    kupigania haki za Wanawake na uhuru wao katika jamii,
c.    kuelekeza juhudi na mapambano yetu kuhusu Haki ya Usawa na kuheshimu utu wa wengine,
d.    kushinikiza watawala kuhusu utawala bora ili kupambana na rushwa na ufisadi,
e.    kushinikiza uwepo wa haki kuhusu masuala ya Tabianchi na Mazingira.
Hivyo basi, mnamo tarehe 25 Mei 2017 jijini Dar es salaam, kampeni ijulikanayo kama “Africans Raising Initiative” chini ya Actionaid Tanzania na Activista Tanzania ilizinduliwa katika kilele cha maadhimisho ya “Siku Ya Ukombozi Wa Mwafrika”-“African Liberation Day”.










Kampeni ya “Africans Raising Initiative” imekuja ikiwa na kauli mbiu “Africans Raising for Justice, Peace and Dignity” ikimaanisha “Waafrika Waamke Kutetea Haki zao, Amani na Utu wao”.
Uzinduzi wa Kampeni hiyo uliambatana na tamasha la jioni kwa Vijana lililofanyika katika kituo cha mafunzo, ubunifu na sanaa kwa watoto na vijana-Kigamboni Community Centre (KCC) kama inavyoonekana katika picha.
Picha zote: Activista-Tanzania
Makala hii imeandaliwa kwa msaada wa Ripoti ya Makubaliano ya Mkutano.

Imetolewa na Jielimishe Kwanza Blog